12.20.2015

kadesha na matukio: Kichekesho cha mbwa

download hapa;

kadesha na matukio: Kichekesho cha mbwa

 James ze navigator

Kichekesho cha mbwa

https://youtu.be/updJrzKYNQ4

James ze navigator

Rais Magufuli amtumia salamu za Rambirambi Rais Kikwete kwa kufiwa na Dada yake

James ze navigator
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye amepatwa na msiba mzito wa kufiwa na Dada yake Mpendwa Bi. Tausi Khalfan Kikwete kilichotokea jana tarehe 17 Desemba, 2015 huko nchini India.
Katika salamu hizo, Rais Magufuli amesema anaungana na familia ya Rais Mstaafu Kikwete katika kipindi hiki kigumu cha majonzi ya kuondokewa na mtu muhimu kwa familia.
"Kwa masikitiko makubwa nakupa pole nyingi Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete kwa kufiwa na dada yako ambaye alikua nguzo muhimu katika familia" Amesema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amemuomba Rais Mstaafu Kikwete kumfikishia salamu nyingi za pole kwa familia nzima na amewaomba wawe na moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Rais Magufuli amemuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema aipumzishe roho ya marehemu Tausi Khalfan Kikwete mahali pema peponi, Amina.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Afanya Ziara Katika Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi jijini Dar.......Aagiza Yaanze Kufanya Kazi Ifikapo Januari 10 Mwakani 

James ze navigator


Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (BRT) utaanza Januari 10, 2016.Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa wakati akikagua ujenzi wa miundo mbinu ya Mradi wa Mabasi yaendayo haraka leo jijini Dar es Salaam.

Pia Majaliwa amewaagiza watendaji wizara ya Tamisemi ambao ni wamiliki wa mradi huo kusimamia vyema ili uanze kufanya kazi kama ilivyo pangwa kwa kuwa mabasi 120 yalishawasili jijini Dar es Salaam.
 
Waziri Mkuu ameanza kwa kukagua vituo vya mradi huo kuanzia cha Feri, Jangwani, Kimara na kumalizia na Morocco na kuwapongeza kwa kumaliza kujenga vituo 15 kati ya 27 na amewaagiza kumalizia vituo vilivyo baki ili kufikia januari 10 mwakani mabasi yaanze kufanya kazi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akisalimiana na watendaqji mbalimbali wa mradi wa mabasi yaendayo haraka waliofika katika kituo cha Feri cha Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (BRT) leo jijini Dar es Salaam. 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha Feri jijini Dar es Salaam leo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akipanda basi la mwendo wa haraka mara baada ya kutembelea maeneo mbalimbali katika kituo cha feri leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa katika kituo cha Mradi wa mabasi cha Jangwani kukagua maendeleo ya ujenzi ya kituo hicho ikiwa ujenzi wa kituo hicho upo hatua za mwisho kukamilika 
by james ze navigator

James ze navigator

UVCCM yampa tano Rais Magufuli


UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umesema unaunga mkono kasi ya utekelezaji kazi wa serikali ya awamu ya tano, chini ya Rais John Magufuli na kwamba anachofanyika sasa ndio kiu ya Watanzania.
Aidha umoja huo umesema utaendelea kumuunga mkono kila hatua kwa lengo la kuona vijana wote wa Tanzania wanarudi katika ari ya uwajibikaji kama ilivyokuwa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza.
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuongoza ufanyaji usafi katika eneo la Soko la Kigogo, Dar es Salaam.
“Kinachofanywa sasa na serikali ya CCM ya awamu ya tano ni matokeo ya ubora wa sera zilizomo kwenye ilani yake ya uchaguzi, tumeahidi, tumedhamiria na sasa tunatimiza ahadi za Chama,” alisema Shaka.
Shaka alikuwa akijibu swali aliloulizwa kama yanayotekelezwa sasa na serikali ya awamu ya tano, yanatokana na ilani ya uchaguzi ya CCM. Kwa mujibu wa Shaka, UVCCM itaendelea kumuunga mkono kwa vitendo Dk Magufuli katika dhamira na malengo ya serikali yake, hasa kupiga vita rushwa, maonevu, ubadhirifu wa mali za umma, mkakati wa udhibiti na matumizi bora ya rasilimali na maliasili za Taifa pamoja na kuhimiza uwajibikaji maeneo ya uzalishaji mali.
“Tutamuunga mkono kwa hali na mali, tutawakabili na ikibidi kuwaumbua watakaothubutu kumsakama au kumkwamisha, tunahitaji kasi ya kuwatumikia wananchi ili nchi ipige hatua zaidi kiuchumi, “alisema.
Kuhusu kasi yake serikali yake katika kuwachukulia hatua watendaji wazembe, kuwaweka kando wale tuhuma za ufujaji na wizi wa fedha za serikali, Shaka amesema wakati wa kubebana umekwisha na sasa ni kazi kwenda mbele.
“Ulikuwa ni mwezi mmoja wenye maajabu, matumaini na mararajio katika utendaji wa Serikali inayotumikia wananchi wake, tunataka Dk Magufuli zaidi kutumbua zaidi majipu na kusafisha uchafu, “alisisitiza Shaka.

Shule 11 kutohusika elimu bure


WIZARA ya Elimu, Sayansi na Ufundi imetoa waraka wa elimu kuhusu elimumsingi bila malipo na kutoa orodha ya shule za msingi 11 za Serikali ambazo hazihusiki na utoaji wa elimu bure uliotangazwa na Rais John Magufuli. Elimumsingi inajumuisha elimu ya awali, ya msingi na sekondari ambayo itaanza Januari mwakani.
Katika Waraka Elimu Namba 6 wa Mwaka 2015 kuhusu utekelezaji wa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, wizara hiyo imetaja shule hizo kuwa ni Shule ya Msingi Olympio (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Diamond (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Oysterbay (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Iringa (Iringa) na Shule ya Msingi Mkapa (Mbeya).
Nyingine ni Shule ya Msingi Angaza (Mbeya); Shule ya Msingi Nuru (Mbeya); Shule ya Msingi Lupilisi (Ruvuma); Shule ya Msingi Tanga (Tanga); Shule ya Msingi Arusha (Arusha) na Shule ya Msingi Kisimani iliyoko mkoani Arusha.
Wizara hiyo pia imesema waraka huo hauzihusu shule zinazomilikiwa na mashirika ya umma ama taasisi za umma ambazo zinaendeshwa kwa taratibu sawa na shule za binafsi. Katika waraka huo, wizara hiyo imetoa majukumu yanayotakiwa kufanywa na Wizara hiyo, Tamisemi, wakurugenzi wa manispaa na halmashauri ya wilaya, wakuu wa shule, bodi za shule, wazazi na wananchi.
Majukumu ya wazazi na walezi Kuanzia Januari, wazazi wanatakiwa tu kununua sare za shule na michezo, vifaa vya kujifunzia vikiwemo madaftari na kalamu, na chakula kwa wanafunzi wa kutwa na kugharimia matibabu kwa watoto wao.
Wanatakiwa pia kulipia nauli ya kwenda shule na kurudi kwa wanafunzi wa kutwa na wanafunzi wa bweni wakati wa likizo; kununua magodoro, shuka, vifaa vya usafi binafsi kwa wanafunzi wanaosoma shule za bweni na wanaoishi katika hosteli zinazotumiwa na serikali; na kukemea na kutoa taarifa kuhusu mienendo inayokwenda kinyume na elimumsingi bila malipo.
Wazazi na wananchi wengine pia wanatakiwa kuendelea kujitolea nguvukazi na mali ili kuleta ustawi na maendeleo ya shule zilizoko ndani ya jamii.
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Katika waraka huo, Wizara ina jukumu la kutenga fedha za kugharimia utayarishaji na uendeshaji wa mitihani ya kitaifa kulingana na idadi ya wanafunzi; kutenga fedha kwa ajili ya Uthibiti Ubora wa Shule na kutenga fedha za kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utoaji wa elimumsingi bila malipo na kuchukua hatua stahiki pale inapobidi.
Inachotakiwa kufanya Tamisemi Kwa upande wa Tamisemi, waraka huo unaielekeza wizara hiyo kutoa miongozo ya matumizi ya fedha za umma kwa wakuu wa shule, kuratibu uandaaji wa mipango na bajeti ili kupata mipango na bajeti ya taifa kila mwaka inayozingatia mahitaji halisi ya elimumsingi bila malipo.
Pia Tamisemi inatakiwa kufanya ukaguzi wa ndani, ufuatiliaji na tathmini za mara kwa mara ili kuhakikisha elimumsingi bila malipo inatolewa kwa ufanisi na viwango vya ubora inavyostahili.
Kuratibu utoaji mipango na bajeti za ruzuku ya uendeshaji wa shule ikiwemo ulinzi, umeme, maji na ununuzi wa chaki na karatasi pamoja na vifaa vingine vya kufundishia na kujifunzia.
Kutenga na kutuma fedha shuleni kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wa mitihani na majaribio mbalimbali shuleni ikiwemo tathmini endelezi, kununua vitabu, kemikali na vifaa vya maabara, samani yakiwemo madawati, vifaa vya michezo, matengenezo ya mashine na mitambo pamoja na kujenga na kukarabati miundombinu ya shule.
Kutenga na kutuma fedha shuleni za kugharimia wanafunzi wenye mahitaji maalumu waliopo kwenye shule na vitengo vya elimu maalumu kwa kuwapatia chakula yaani mlo mmoja kwa wanafunzi wa kutwa na milo mitatu kwa wanafunzi wa bweni pamoja na vifaa na visaidizi.
Wakuu wa shule Waraka huo unawataka wakuu wa shule kuwapa maelekezo wazazi kuhusu aina ya vifaa vinavyohitajika mfano rangi ya kitambaa cha sare ya shule, sare za michezo, idadi na aina ya madaftari watakayotumia wanafunzi ili wazazi wanunue wenyewe.
Pia wanatakiwa kusimamia na kuhakikisha fedha inayotolewa na Serikali inatumika kama ilivyokusudiwa kulingana na taratibu za fedha za Serikali na kutoa takwimu na taarifa sahihi za idadi ya wanafunzi na mahitaji mengine ya shule.
Kamati au Bodi za Shule Wizara katika waraka huo inataka kamati za shule kufuatilia na kusimamia matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali ili ziweze kuleta tija; kuhakikisha kuwa sera, nyaraka, maelekezo na miongozo ya Serikali inazingatiwa na kutoa ushauri stahiki.
Kuwashirikisha wazazi, walezi, walimu na wanafunzi katika maamuzi na maazimio ya masuala mbalimbali yanayohusu maslahi na maendeleo ya shule kwa ujumla.
Pia waraka huo umeainisha majukumu ya walimu ambao kazi yao kubwa ni kusimamia sera na miongozo ya utoaji wa elimu bure. Wanafunzi ambao ndio walengwa wakuu wa utoaji wa elimu pia wametakiwa kuhakikisha wanakuwepo shule katika kipindi chote cha masomo.

CDA wabomoa nyumba 140 Dodoma

ZAIDI ya nyumba 140 mjini Dodoma zimebomolewa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kutokana na wananchi kujenga kiholela katika maeneo yasiyoruhusiwa huku Jeshi la Polisi likilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliokuwa wakileta fujo ikiwemo kufunga barabara kuu ya Dodoma – Singida.
Bomoabomoa hiyo imefanyika katika maeneo ya Chinangali, Ndachi, Barabara ya Bahi na Kizota Dampo katika eneo la Kizota licha ya kutolewa notisi ya siku saba kwa wananchi hao kuondoka, lakini walikaidi amri hiyo ndipo Jeshi la Polisi pamoja na watendaji wa CDA walianza kazi hiyo.
Hata hivyo, wananchi ambao hawakukubaliana na kazi hiyo, walianza kuwarushia polisi mawe.
Baadhi ya wakazi waliangua vilio wengine wakipoteza fahamu baada ya kushuhudia nyumba zao zikibomolewa.
Wakizungumza nje ya nyumba zao, baadhi ya wananchi walisema kazi hiyo ni ya ghafla na hawakupewa taarifa na hawaelewi hatma ya maisha yao kwani hawana pa kulala.
Mkazi wa Kizota Dampo, Mwajuma Khamis alisema alikuwa akitegemea nyumba hiyo kwa ajili ya makazi na sasa hana pa kwenda kufuatia bomoabomoa hiyo.
Mkazi mwingine wa Kizota Dampo, Evania Joseph alisema hawakupewa taarifa yoyote juu ya ubomoaji huo na umefanyika ghafla na kuwaweka katika wakati mgumu.
Kwa upande wake, Ofisa Habari na Mahusiano wa CDA, Angela Msimbila alisema kazi hiyo ni endelevu ambapo wananchi hao walipewa notisi ya siku saba, lakini wamekaidi amri hiyo.
Alisema wananchi walijenga kwenye maeneo yasiyoruhusiwa hali iliyofanya mamlaka hiyo kutekeleza kazi ya ubomoaji.
Wakati kazi hiyo ikiendelea kufanyika katika maeneo mengine, baadhi ya wananchi waliamua kuchukua sheria mkononi na kufunga barabara kuu ya Dodoma-Singida ndipo Polisi ikalazimika tena kwenda na kuwatawanya wananchi hao waliofunga barabara huku mabomu ya
James ze navigator
Majaliwa ataka mabasi ya kasi yawe barabarani
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, ameagiza Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kuhakikisha Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), unaanza kufanya kazi Januari 10, mwakani. Kadhalika, ameagiza wizara hiyo kupitia upya mikataba ya wadau wa mradi huo, wakiwemo Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) na wadau wengine kwenye mradi huo, ili kurekebisha kasoro zilizopo kwa lengo la kuhakikisha Serikali inanufaika.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema hayo Dar es Salaam jana, wakati akikagua vituo vya mradi huo kuanzia eneo la Kivukoni hadi Kimara na kisha kituo cha Morocco, Kinondoni. Alisema kati ya vituo vya kupakia na kushukia abiria 27 vya mradi huo, vituo 15 viko kwenye hatua za mwisho za kukamilika, hivyo kuitaka wizara hiyo kuhakikisha Januari 10, mwakani, mradi huo unaanza kazi kwa vituo vilivyokamilika.

“Vituo vikuu vitano lazima vianze kazi Januari 10, mwakani na kasoro zilizopo zifanyieni marekebisho, ikiwemo kubadilisha vigae kwenye baadhi ya vituo kama kile cha Kivukoni, kazi hiyo ifanyike kwa wakati na nitarudi tena mwisho wa mwezi huu, kukagua kabla mradi haujaanza kazi,” alisema Majaliwa.

Alivitaja vituo vikuu vitano vitakavyotakiwa kuanza kazi Januari 10 kuwa ni Kimara, Ubungo, Morocco, Kariakoo na Kivukoni.

Akizungumzia kasoro za vigae kwenye kituo cha Kivukoni, Waziri Mkuu Majaliwa alisema vigae vilivyotumika si sahihi na viko chini ya kiwango na kumtaka mkandarasi kuanza kuvivunja na kuweka vingine vyenye ubora, vitakavyokuwa rafiki kwa wasafiri.

Kuhusu kupitia upya mikataba ya wadau wa mradi huo, Waziri Majaliwa alimwagiza Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene, kupitia upya mikataba iliyoingiwa baina ya wadau hao na kuhakikisha kasoro zilizopo zinafanyiwa kazi kabla ya mradi kuanza, ili Serikali inufaike na mradi huo.

Alisema pamoja na kufanyiwa marekebisho hayo, pia Wizara inapaswa kuthamini wadau wa daladala, ambao mara baada ya kuanza kwa mradi huo, magari yao yatakosa kazi, hivyo waangalie jinsi ya kuwaingiza kwenye mradi kwa wale wenye sifa.

“Mradi huu utakapoanza, ina maana daladala zitaondoka barabarani, sasa Wizara ithamini wadau hao na wenye sifa muwaingize kwenye mradi ili kuondoa malalamiko yasiyo na msingi,” alisema Majaliwa. Aliongeza kuwa, Serikali kama mwendeshaji wa mradi huo, imetoa fursa kwa wawekezaji kutoa huduma za usafiri na kwamba ni vyema mfumo wa tiketi ambao umeshafungwa na mwekezaji, uchunguzwe na Serikali ili kudhibiti mapato.

Alisema kabla ya mradi huo kuanza kazi, Wizara na mamlaka husika zitatakiwa kuingia mikataba na wawekezaji wa mradi huo, ili kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake na watakaoshindwa wawajibike.

Majiko ya feri Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa ameagiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Manispaa ya Ilala, kubadilisha mfumo wa majiko yanayotumika kukaangia samaki eneo la Feri na kuweka ya kisasa yatakayodhibiti moshi.

Alisema hivi sasa hali si shwari eneo la Feri kutokana na eneo lote kuzingirwa na moshi, ambao licha ya kuathiri wafanyabiashara sokoni hapo, lakini pia unaharibu mazingira na miundombinu jirani. “Huu moshi udhibitiwe, maana hata hapa mmesikia ninakuja, mkapiga deki, vinginevyo moshi ulikuwa umejaa. Sasa huu ni uharibifu kwa miundombinu, wekeni majiko mapya ya kisasa yasiyotoa moshi, hatuwezi kuendelea kwa moshi huu,” alisema Majaliwa.

Akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Miradi kutoka Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Crispinus Ako, Waziri Mkuu alimtaka kusimamia maelekezo yote aliyotoa na kuhakikisha yanatekelezwa kwa wakati.

Agizo lingine la Waziri Mkuu katika kituo cha Kivukoni ni kwa Mkurugenzi huyo pamoja na viongozi wengine, kusimamia ujenzi wa uzio kwenye eneo hilo, ili kudhibiti matukio ya wizi ndani ya kituo hicho. Alisisitiza uwepo wa utaratibu wa kuingia na kutoka kwa mabasi yaletayo na kupakia abiria wanaoshuka kwenye mabasi yaendayo kasi, ili kue

MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SEKONDARI KIDATO CHA TANO

UPDATES:HIZI HAPA JOINING INSTRUCTIONS ZOTE ZA FORM V/KIDATO CHA TANO(5) 2017/2018   MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SEKONDARI...